Watu 100 wauwawa na Boko Haram Nigeria
Wanamgambo wa kundi la Boko Haram wanaripotiwa kuwauwa watu kadhaa katika mashambulio kaskazini mashariki mwa Nigeria. Nyumba pia zilichomwa katika wimbi la hivi karibuni la mashambulizi katika jimbo la Borno. Hali hiyo inakuja baada ya kundi hilo la itikadi kali ya Kiislamu kuuteka mji wa Baga mwishoni mwa juma. Mkuu wa wilaya ya Baga, Abba Hassan amesema kiasi ya watu 100 wamefariki wakati wanamgambo hao walipoudhibiti mji, ambao uko katika ukingo wa ziwa Chad. Kiasi ya vijiji 16 vimeshambuliwa katika eneo hilo tangu wakati huu. Mashambulio hayo yametokea wakati rais Goodluck Jonathan amezindua kampeni ya kutaka kuchaguliwa kuwa rais mwezi Februari. Kundi la Boko Haram limekuwa likifanya kampeni ya kigaidi kwa zaidi ya miaka mitano sasa katika juhudi za kuunda taifa la Kiislamu.
Msako unaendelea kuwatafuta wauaji wa watu 12Katika shambulio lililotokea katika ofisi za jarida la Charlie Hebdo mjini Paris siku ya Jumatano. Polisi wanatafuta katika maeneo ya vijijini watuhumiwa wawili, Cherif na Said Kouachi, ambao wanaripotiwa wamefanya uporaji katika kituo kimoja cha petroli. Ufaransa umekuwa na siku ya kwanza ya maombolezo jana Alhamisi ikiwakumbuka wale waliopoteza maisha katika mauaji hayo, ikiwa ni pamoja na polisi mwanamke ambaye alipigwa risasi mtaani.
Maafisa nchini Ufaransa wamesema hakuna ushahidi wa uhusiano kati ya mauaji ya Charlie Hebdo na shambulio la pili siku ya Alhamisi. Polisi mwanamke alipigwa risasi katika eneo la Montrouge kusini mwa mji mkuu Paris
Yatsenyuk akutana na Merkel mjini Berlin
Yatsenyuk akutana na Merkel mjini Berlin
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amesema vikwazo dhidi ya Urusi vitaondolewa tu pale ambapo makubaliano ya amani yatatekelezwa na pande zote mbili katika mzozo huo nchini Ukraine. Merkel ametoa matamshi hayo wakati wa mkutano wa pamoja na waandishi habari mjini Berlin pamoja na waziri mkuu wa Ukraine Arseniy Yatsenyuk. Chini ya makubaliano ya Septemba mwaka uliopita, Ukraine na waasi wanaoiunga mkono Urusi walikubaliana kusitisha mapigano, lakini yameshindwa kuzuwia mapigano zaidi.
Merkel ameweka msimamo sawa kwa kusema vipengee vyote vya makubaliano ya Minsk ni lazima vitimizwe na mkutano mjini Astana utakuwa na maana kwamba vipengee vyote hivyo vitatimizwa mara moja. Mazungumzo zaidi yamefanyika mwezi Desemba kuweza kupatikana kwa makubaliano ya kusitisha mapigano, hata hivyo, yalivunjika na kusababisha makubaliano ya kubadilishana wafungwa.
http://www.bbc.co.uk/swahili
http://www.bbc.co.uk/swahili
No comments:
Post a Comment